Urusi, Ukraine zashambuliana kwa droni usiku kucha
9 Machi 2025Droni 52 kati ya hizo ziliharibiwa katika eneo la mpaka la Belgorod wakati 13 zilidunguliwa Lipetsk na tisa zilizoangushwa zilikuwa katika anga la mkoa wa Rostov.
Droni zilizosalia zilidunguliwa katika maeneo mengine matano ukiwemo mkoa wa Kursk. Gavana wa eneo la Chuvashia lililo kilomita 1,300 kutoka mpaka wa Urusi na Ukraine Oleg Nikolaye, amesema droni moja ilishambulia jengo la kiwanda. Amesema shambulio hilo halikumjeruhi mtu yeyote.
Soma pia: Urusi yaishambulia tena Ukraine kwa droni
Ukraine kwa upande wake imesema mifumo yake ya ulinzi wa anga imeziteketeza droni 73 kati ya 119 zilizorushwa na Urusi usiku wa kuamkia leo.
Imeongeza kuwa droni 37 kati ya hizo zilipoteza mwelekeo. Kulingana na jeshi la nchi hiyo mikoa sita imeathiriwa na mashambulizi hayo ingawa hakukutolewa ufafanuzi wa haraka kuhusu uharibifu huo.