MigogoroUlaya
Urusi na Uturuki zajadili juhudi za kusitisha vita Ukraine
12 Aprili 2025Matangazo
Wameyafanya majadiliano hayo kando ya mkutano wa diplomasia unaofanyika Antalya kusini mwa Uturuki huku Lavrov akimpongeza Rais wa Marekani Donald Trump kuwa anauelewa mzozo wa Urusi na Ukraine kuliko kiongozi yeyote wa Ulaya.
Soma zaidi: Uturuki yajitolea kuzipatanisha Urusi na Ukraine ili kumaliza vita
Kulingana na chanzo cha kidiplomasia kutoka Uturuki, wawili hao wamejadili pia kuhusu hali ya Bahari nyeusi na mvutano unaoendelea Mashariki ya Kati. Kando ya mizozo, wamezungumza pia kuhusu ushirikiano katika sekta ya nishati, uchumi na masuala mengine yanayolenga kuimarisha uhusiano wa Urusi na Uturuki.