MigogoroUlaya
Urusi na Ukraine washambuliana kwa droni na makombora
8 Februari 2025Matangazo
Urusi kwa upande wake imesema vikosi vyake vimechukua udhibiti wa mji wa kimkakati wa Toretsk katika mkoa wa Donetsk mashariki mwa Ukraine, taarifa iliyokanushwa na jeshi la Ukraine lililoeleza kuwa mapambano makali bado yanaendelea.
Hayo yakiarifiwa, rais wa Marekani Donald Trump amesema yuko tayari kuujadili mzozo wa Ukraine lakini haijawa wazi ikiwa rais wa Urusi Vladimir Putin anayo nia ya dhati ya kushiriki katika mazungumzo hayo.
Wachambuzi wanasema kutokana na mafanikio anayoyapata katika uwanja wa vita, Putin anakaribia kuyafikia malengo yake na hatokuwa na sababu yoyote ya kushiriki mazungumzo ya amani.