Urusi inaendeleza mashambulizi yake mjini Mykolaiv, Ukraine
16 Februari 2025Matangazo
Shambulizi hilo pia linasemekana kuharibu nyumba kadhaa katika eneo la Kiev.
Jeshi hilo limeongeza kuwa Urusi ilirusha droni 143 nchini humo ambazo 95 zilidunguliwa huku 46 zikishindwa kufika katika maeneo zilikolengwa kufuatia mifumo ya kielektroniki iliyotumika.
Ukraine yasema miundombinu yake ya gesi imeshambuliwa
Gavana wa Mykolaiv Vitaliy Kim amesema moto uliokuwepo katika jengo hilo ulifanikiwa kuzimwa. Haikuwa wazi lakini ni miundombinu ya aina gani iliyolengwa katika shambulizi hilo.
Hadi sasa Urusi haijasema chochote kuhusiana na tukio hilo, lakini pande zote mbili Urusi na Ukraine zinakana madai ya kuwalenga raia katika vita hivyo vilivyoanzishwa na Urusi baada ya kumvamia jirani yake takriban miaka mitatu iliyopita.