JamiiUreno
Ureno na Uhispania zakumbwa na tatizo kubwa la umeme
28 Aprili 2025Matangazo
Shirika linaloshughulikia usafiri wa anga barani Ulaya la Eurocontrol, hata hivyo, limesema bado ni mapema mno kusema ni safari ngapi za ndege zimeathirika.
Katika hatua nyingine, shirika la ugavi wa umeme la Ureno, REN, limesema hali ya nadra iliyotokea kwenye anga ya Uhispania kutokana na joto lililokithiri ilisababisha umeme kukatika kwenye rasi ya Iberia, na huenda gridi ya taifa ikarejesha huduma kikamilifu baada ya wiki moja.
Lakini shirika la habari la El Pais la nchini Uhispania limeripoti huduma ya umeme inaweza kurejea baada ya masaa 10, likimnukuu mwendeshaji wa gridi ya umeme nchini humo.