SiasaUreno
Ureno kutafakari ikiwa itaitambua Palestina kama taifa huru
31 Julai 2025Matangazo
Ufaransa, Uingereza na Canada ni mataifa ya hivi karibuni zaidi yaliyotangaza azma hiyo, hatua inayozidisha shinikizo kwa Israel ambayo inaonekana kutengwa kidiplomasia kutokana na operesheni zake huko Gaza.
Azimio nambari 181 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la Novemba 29 mwaka 1947 lilipendekeza kuigawanya Palestina na kuanzisha mataifa mawili huru ya Israel na Palestina ambayo yangelitakiwa kuishi bega kwa bega kwa usalama na amani.