UN yatahadharisha kuhusu hali ya wanaharakati Kongo
5 Machi 2025Lawlor, mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya wanaharakati wa haki za binadamu, ameelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusu hali inayowakabili wanaharakati mashariki mwa Kongo.
Lawlor ameonya kwamba wale ambao wameandika na kushutumu ukiukaji uliofanywa wakati wa vita, pia wamelengwa moja kwa moja.
Wanaharakati wanahitaji kuhamishwa
Katika taarifa, mtaalamu huyo amesema wanaharakati hao wanahitaji msaada sasa ikiwa ni pamoja na kuhamishwa kwa muda pamoja na familia zao.
UN: Wanaharakati mashariki mwa Kongo wanakabiliwa na hatari kubwa
Lawlor, mtaalam huru aliyeidhinishwa na Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa lakini ambaye hazungumzi kwa niaba ya Umoja huo, amesema amepokea maombi mengi ya msaada kutoka kwa wanaharakati walioko mashinani.
Wanaharakati nchini Kongo wanaishi kwa hofu
Mtaalamu huyo ameongeza kuwa wanaharakati hao wanaishi kwa hofu na athari zilizopo ni za wazi, huku akieleza kuwa wapiganaji wa kundi la waasi wa M23 wanaandika orodha ya wanaharakati ili kuwakamata katika maeneo yakioko chini ya udhibiti wao.
UN: Waasi wawateka wagonjwa 130 mashariki mwa Kongo
Pia amesema amepokea ripoti za kuaminika za wanaharakati wa haki kuzuiliwa bila mawasiliano, na kupotezwa kwa nguvu pamoja na kuteswa katika maeneo ya jimbo la Kivu Kaskazini.
Lawlor, amesema kuwa takriban wanaharakati sita wameripotiwa kutoweka walipokuwa wakijaribu kutoroka Goma baada ya kutekwa na waasi wa M23.
Lawlor aliangazia hatari iliyoongezeka kufuatia hatua ya wafungwa wengi kutoroka kutoka jela nyingi mashariki mwa Kongo na kusema maelfu ya wafungwaikiwa ni pamoja na wahalifu wa vurugu na wakuu wa makundi yenye silaha ambao walikuwa wameshtakiwa kwa ukiukaji mkubwa unaojumuisha uhalifu wa kivita na wa kibinadamu walitoroka.
Lawlor ameonya kuwa baadhi yao kwasasa wanatishia haki za wanaharakati waliotoa msaada kwa waathiriwa na mashahidi katika kesi zao.
Wakimbizi wengi wa Kongo watafuta hifadhi Burundi
Shirika la UNHCR limesema kuwa takriban watu 61,000 waliokimbia vita nchini Kongo wametafuta hifadhi nchini Burundi ambayo imewapokea wakimbizi wengi kutoka nchini humo.
Vita Kongo vyasababisha mgogoro mkubwa wa wakimbizi Burundi
Brigitte Mukanga-Eno, mwakilishi wa UNHCR nchini Burundi amesema wamekuwa wakiwapokea wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo katika wiki chache zilizopita lakini idadi kubwa ya wakimbiziilianza kuwasili wikendi ya tarehe 14 Februari ambapo idadi kubwa ya watu walivuka kupitia kwenye Mto Rusizi na kuingia Burundi.
Unyanyasaji mkubwa wafanyika katika mstari wa mbele wa vita
Taarifa ya UNHCR, imesema kuwa karibu na mstari wa mbele wa vita, unyanyasaji wa kijinsia na ukiukwaji wa haki za binadamu bado umekithiri, kama vile uporaji na uharibifu wa nyumba na biashara za raia.