Haki za binadamuAsia
UN yabaini ukiukwaji wa haki za binadamu Bangladesh
12 Februari 2025Matangazo
Turk amesema hayo mbele ya waandishi wa habari alipokuwa akiwasilisha ripoti ya kiuchunguzi mjini Geneva, na kusema huenda kulifanyika uhalifu dhidi ya ubinaadamu, katika mazingira ya hofu na kamatakamata ya idadi kubwa ya watu.
Ushahidi wa maafisa wa Bangladesh na vidhibiti vingine vimeonyesha kulikuwepo na sera rasmi ya kushambulia na ukandamizaji mkubwa dhidi ya waandamanaji waliopinga serikali pamoja na waliowaunga mkono.
Soma pia:UN yasema kuna hatari ya vita vya Kongo kuvuka mipaka
Ofisi hiyo imeomba kufanyika uchunguzi wa haraka.
Maandamano hayo yaliyoongozwa na wanafunzi waliolalamikia sekta ya ajira, yaliligubika taifa hilo na kusababisha aliyekuwa Waziri Mkuu Sheikh Hasina kujiuzulu.