MigogoroMashariki ya Kati
UN: Mauaji ya wahudumu wa afya Gaza "uhalifu wa kivita"?
4 Aprili 2025Matangazo
Volker Turk amesema mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa ameshtushwa na mauaji ya hivi karibuni ya wahudumu wa afya 15 na wafanyakazi wa mashirika ya kibinaadamu ambao miili yao ilikutwa katika kaburi la pamoja karibu na mji wa kusini mwa Gaza wa Rafah.
Soma pia: Jeshi la IDF kuchunguza vifo vya wafanyakazi wa misaada Gaza
Turk ametoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi wa kina, huru na wa haraka kuhusu tukio hilo la Machi 23 ambalo maafisa wa Israel walishambulia gari ya kubeba wagonjwa wakidai kuwa walikuwa wakiwalenga "magaidi."