MigogoroHaiti
UN: Magenge ya wahalifu yamejiimarisha Haiti
25 Juni 2025Matangazo
Wataalamu hao waliopewa dhamana ya kufuatilia vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya magenge hayo, wameelezea wasiwasi wao kuhusu kuenea kwa ghasia katika nchi hiyo masikini ya Carribean yenye serikali ya mpito iliyo dhaifu, isiyokuwa na rais, bunge na yenye jeshi la polisi lililoelemewa, wakisisitiza kuwa magenge hayo yamekuwa na silaha zenye ubora licha ya kuwekewa vikwazo.
Umoja wa Mataifa umesisitiza kuwa licha ya kutumwa kwa kikosi cha kimataifa cha kulinda amani ambacho kinakabiliwa na matatizo ya fedha na vifaa, hakuna maendeleo makubwa yaliyoshudiwa huko Haiti katika kurejesha hali ya utulivu na utawala wa sheria.