UN: Kambi ya Zamzam nchini Sudan yakaribia kuwa tupu.
25 Aprili 2025Matangazo
Katika taarifa, OCHA imesema kambi hiyo ya wakimbizi ya Zamzam ambayo ilikuwa makazi ya takriban wakimbizi 400,000 kabla ya wengi kutoroka, imebaki na idadi ndogo mno ya wakimbizi.
Mashirika ya misaada yalaani shambulizi dhidi ya kambi ya wakimbizi Sudan
OCHA imeongeza kuwa picha za setilaiti zilionyesha moto ulioenea, huku wanamgambo hao wakiripotiwa kuwazuia wakimbizi wengine kuondoka.
Pia imesema wakimbizi hao kutoka Zamzam sasa wanaelekea katika maeneo mengine na takriban 150,000 wamewasili katika eneo la Al Fasher huku wengine 181,000 wakielekea Tawila.