UN: Haiti huenda ikakabiliwa na ghasia zaidi
22 Aprili 2025María Isabel Salvador amesema ukubwa wa ghasia nchini Haiti umezua hofu miongoni mwa wakazi wa nchi hiyo na kwamba wanaogopa kuanguka kabisa kwa serikali yao chini ya shinikizo la makundi ya uhalifu.
Polisi yarejesha udhibiti baada ya genge kuwafungulia wafungwa 500 Haiti
Salvador ameonya kuwa huenda Haiti ikikabiliwa na machafuko makubwa ikiwa hakutaongezwa ufadhili na msaada kwa kikosi cha kimataifa kinachoongozwa na Kenya nchini humo kuisaidia polisi kukabiliana na magengehayo na kuzuia kuenea kwa vurugu katika maeneo mengine nje ya mji mkuu Port-Au-Prince.
Salvador pia amesema hivi karibuni, magenge hayo yaliteka mji wa Mirebalais katikati mwa Haiti na wakati wa shambulizi hilo, zaidi ya wafungwa 500 walitoroka jela, hali inayozidisha hofu.