Umoja wa Ulaya kuipa Misri msaada wa euro bilioni nne
20 Mei 2025Matangazo
Umoja wa Ulaya umesema utaipa Misri msaada mwingine zaidi wa thamani ya euro bilioni nne katika mfumo wa mikopo ili kuiwezesha serikali ya mjini Cairo ikidhi baadhi ya mahitaji yake ya kifedha, pamoja na mpango maalum wa mkopo wa Fuko la Fedha la Kimatiafa IMF uliopo.
IMF yashusha makaridio ya ukuaji wa uchumi wa dunia
Makubaliano ya awali kuhusu msaada huo wa Umoja wa Ulaya yaliafikiwa kati ya baraza la umoja huo linaloziwakilisha nchi wanachama na bunge la Ulaya.
Taasisi hizo mbili zinatakiwa kutia saini ili kuyafanya makubaliano hayo yawe rasmi kabla kiwango cha kwanza cha fedha kutolewa.